Wajumbe wa kamati ya utendaji ya Simba watakutana
leo kumjadili kocha mpya waliomtangaza.
Kocha mpya aliyetangazwa na Simba ni Zdravko
Logarusic raia wa Croatia na aliwahi kuwa kocha wa Gor Mahia ya Kenya.
Wakati wakiwa wamemtangaza kocha mpya, mwenyekiti
waliyemsimamisha, Aden Rage alitangaza kuwarejesha Abdallah Kibadeni na Jamhuri
Kiwhelo ‘Julio’.
Lakini aliyetangazwa kuwa Kaimu Mwenyekiti wa Simba,
Swed Nkwabi amesema suala hilo watalijadili lakini pia watajadili masuala mengine kadhaa.
“Tutakutana na kulijadili suala hilo kwanza kabla ya
kutoa mustakabari, hivyo tunaomba mvute subira,” alisema Nkwabi.
0 COMMENTS:
Post a Comment