Kocha mkuu wa Yanga, Ernie Brandts
ametaka kikosi chake kuendelea kufunga wastani mzuri wa mabao ili kujiwekea
akiba.
Brandts raia wa Uholanzi amesema wastani
mzuri wa mabao huwa na faida kubwa hasa linapofikia suala la kuwania ubingwa.
“Mabao ni kitu muhimu sana, kama unapata
pointi basi ni vziuri kupata mabao mengi.
“Utaona katika mechi kama nne hivi
tumekuwa na wastani mzuri wa kufunga mabao.
“Angalau matatu kila mechi, huu ni
mwendo mzuri ambao nimeusisitiza zaidi kwa wachezaji.
“Utaona umuhimu wa mabao mnapofikia
mwisho wa ligi, nimezungumza na wachezaji wangu na kuwaeleza hili,” alisema
Brandts.
0 COMMENTS:
Post a Comment