Mshambuliaji wa Simba, Amissi Tambwe
amesema anataka kuendelea kubaki kileleni kwa wafungaji wa Ligi Kuu Bara.
Tambwe ambaye anaongoza kwa mabao ya
kufunga amesema atajituma kufunga mabao mengine zaidi ili kuendelea kubaki
kileleni.
Mrundi huyo ana mabao tisa ambayo hakuna
mshambuliaji mwingine wa timu 13 aliyefikia.
Lakini anafukuzwa kwa karibu na Hamisi
Kiiza wa Yanga ambaye alimfikia alipokuwa na mabao manane kabla ya kufunga la
tisa dhidi ya Kagera Sugar.
Tambwe amekuwa hana mbwembwe sana lakini
uwezo wake wa kufunga mabao umekuwa ni mkubwa sana.
0 COMMENTS:
Post a Comment