Kiungo Athumani Idd ameshindwa kufanya
mazoezi kutokana na kuwa mgonjwa, wakati beki Mbuyu Twite pia hakutokea
mazoezini.
Katika mazoezi ya mabingwa hao kwenye
Uwanja wa Loyola, Chuji, Twite pamoja na beki wa kulia, Juma Abdul walishindwa
kufanya mazoezi.
Abdul peke yake pamoja na Salum Telela
ndiyo walifika mazoezini hapo na kuzungumza na daktari wa timu hiyo, Nassor
Matuzya.
“Chuji, Twite pia wameshindwa kutokea
leo, lakini naendelea kufuatilia afya zao kwa karibu,” alisema daktari huyo.
Hata hivyo alichukua zaidi ya dakika 10
akizungumza na Abdul na Telela kutaka kujua afya zao kabla ya kujiunga na
wenzao.
0 COMMENTS:
Post a Comment