Makamu mwenyekiti wa zamani wa Simba,
Geofrey Nyange ‘Kaburu’ amekuwa kati ya wadau ambao hawakosi mazoezi ya Taifa
Stars.
Kaburu anayejulikana kwa ukali wa
usajili, hakosekani kwenye mazoezi ya Stars inayojiandaa kucheza na Kenya,
Jumanne.
Sasa ni mmoja wa wajumbe wa kamati ya
utendaji ya TFF na amekuwa akisifiwa kwa kuwa karibu na timu, mfano mzuri
wakati yuko Simba.
Ila wakati mwingine Kaburu naye mazoezi
hata haangalii sana, yuko na simu tu. Sijui anawasiliana na nani, au anahifadhi
data za wachezaji waliomvutia.
0 COMMENTS:
Post a Comment