Mashabiki wengi waliojitokeza kwenye
mazoezi ya Taifa Stars inayojiandaa kucheza mechi ya kirafiki na Kenya,
Harambee Stars, walionyesha kuvutiwa zaidi na kiungo Mwinyi Kazimoto.
Kazimoto amerejea katika mazoezi ya
Stars baada ya msamaha wa Kocha Kim Poulsen kwa kuwa alitoroka na kwenda
kufanya majaribio kabla ya kujiunga na Al Markhiya ya daraja la pili nchini Qatar.
Lakini gumzo la leo lilikuwa ni namna
alivyong’ara uso wake na rangi ya ngozi yake na wengi walikuwa wakisema ‘amkwiva’
utafikiri alikuwa Ulaya.
“Utafikiri anaishi Ulaya, au lile joto
la Uarabuni,” alisema shabiki mmoja huku wengine wakimsikiliza kwa umakini na
mjadala ukaendelea.
0 COMMENTS:
Post a Comment