Kuonyesha kuwa mazoezi hayana mchezo, wachezaji wa
Yanga wamekuwa wakicheza kwa nguvu sana.
Mshambuliaji wa Yanga, Hussein Javu alinusurika
kuumia baada ya kiatu cha Nizar Khalfan kumjeruhi kwenye paja.
Kutokana na Nizar kuruka na mguu wake kutua kwenye
paja lake, Javu alitumia kama dakika nzima akijikagua na akashindwa kuendelea
hadi alipopewa matibabu.
Hata hivyo, baadaye Nizar alionekana akimuomba Javu
msamaha na kumueleza kuwa ilikuwa ni bahati mbaya.
Chini ya Ernie Brandts, Yanga wamefanya mazoezi leo
kwenye Uwanja wa Bora jijini Dar es Salaam kujiandaa na Ligi Kuu Bara mzunguko wa
pili utakaoanza Januari, mwakani.
0 COMMENTS:
Post a Comment