Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts ametaka wachezaji
wote wasiokuwa kwenye vikosi vya timu ya taifa wajiunge na timu yake mazoezini.
Brandts amewataka wachezaji ambao hawajaonkana
mazoezini kufika mara moja.
“Kila mchezaji ambaye hajaitwa kwenye kikosi cha
timu ya taifa anatakiwa mara moja kufika mazoezini na kuungana na wenzake.
“Napenda kuona utaratibu wa mazoezi unafuatwa na kila mchezaji afike mara
moja,” alisema Brandts akiwaeleza baadhi ya maofisa wa benchi la ufundi mara
baada ya Yanga kumaliza mazoezi kwenye Uwanja wa Bora Kijitonyama, leo.
Baadhi ya wachezaji ambao hawakuwa wametokea
mazoezini ni Mbuyu Twite na Didier Kavumbagu ambao hawajaitwa kwenye timu zao
za taifa.
0 COMMENTS:
Post a Comment