November 22, 2013





Klabu ya Simba inahitajika kumlipa Abdallah Kibadeni shilingi milioni 18 kutokana na kuvunja mkataba wake wa kuinoa timu hiyo, imefahamika.


Jumanne ya wiki hii Simba ilitangaza kumtimua kocha huyo pamoja na msaidizi wake, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, ambapo nafasi zao zimechukuliwa na Zdravok Logarusic raia wa Croatia na Seleman Matola.

Taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo zinaeleza kuwa Kibadeni ambaye alikuwa akilipwa mshahara wa Sh milioni tatu kwa mwezi, alikuwa amebakisha mkataba wa miezi sita, hivyo kwa kuwa Simba imeuvunja mkataba wake, itatakiwa imlipe kiasi cha Sh milioni 18 ambacho ni malipo ya miezi sita.

“Baada ya mkataba wake kuvunjwa, Kibadeni anatakiwa kulipwa shilingi milioni kumi na nane, maana alikuwa analipwa milioni tatu kwa mwezi na alikuwa amebakisha miezi sita katika mkataba wake,” kilisema chanzo.

Gazeti hili lilipomuuliza Kibadeni juu ya suala hilo, alisema: “Nasubiri barua yao ya kiofisi ya kuvunja mkataba kisha ndiyo nitajua juu ya haki yangu ya malipo,” alisema Kibadeni.

SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic