November 22, 2013





Katika kuhakikisha nidhamu ya timu inaongezeka, uongozi wa Mbeya City umeweka sheria ya wachezaji kutonyoa staili ya kiduku kwenye timu yao.


Kocha mkuu wa Mbeya City, Juma Mwambusi, alisema huo ni mpango wa kinidhamu ambao viongozi wao wameuweka kuhakikisha nidhamu inapewa kipaumbele.

Mwambusi alisema mchezaji yeyote atakayeenda kinyume cha maadili basi hataruhusiwa kuendelea na timu yao, lengo ni kutimiza malengo yao waliyojiwekea ikiwemo kumaliza Ligi Kuu Bara wakiwa katika nafasi nzuri.

“Uongozi na timu kwa jumla tuna malengo yetu tuliyojiwekea mara baada ya kupanda daraja, tunataka kufika mbali kwenye msimu huu wa ligi kuu na kutokana mikakati tuliyoiweka ninaamini tutafanikiwa.

“Tumeanza kutengeneza nidhamu kwenye timu kwa kuwapiga marufuku wachezaji wetu kunyoa kiduku na mitindo mingine yote ya nywele.  Huo ni utaratibu tulioupanga, ni vema ikatambulika hivyo,” alisema Mwambusi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic