Kocha
Mkuu wa timu ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars), Kim Poulsen amesema timu yake
iko tayari kwa michuano ya Chalenji.
Stars
imewasili salama Nairobi, Kenya tayari
kwa mashindano ya Kombe la Chalenji yanayoanza kesho (Novemba 27 mwaka huu)
katika Uwanja wa Nyayo.
Poulsen amesema wamejiandaa
vema na wana matarajio makubwa ya kufanya vizuri.
“Lazima
kutakuwa na upinzani mkubwa lakini lengo ni kufanya vizuri,” alisema.
Kilimanjaro
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iliwasili saa 3 usiku kwa
ndege ya RwandAir, na imefikia katika hoteli ya Sandton iliyoko katikati ya
Jiji la Nairobi.
Kwa
mujibu wa programu ya Kocha Mkuu Kim Poulsen, Kilimanjaro Stars leo (Novemba 26
mwaka huu) ni mapumziko ambapo kesho itafanya mazoezi kujiandaa kwa mechi yake
ya kwanza dhidi ya Zambia itakayochezwa Novemba 28 mwaka huu Uwanja wa Machakos.
0 COMMENTS:
Post a Comment