KISAKA (KULIA) AKIWA NA KOCHA WA ZAMANI WA SIMBA, PATRICK LIEWIG NA MENEJA, MOSES BASENA |
Kocha wa makipa wa Simba, James Kisaka
bado anakumbukwa kutokana na uwezo wake mkubwa aliokuwa nao wakati akiwa kipa.
Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho la
Soka la Kenya (FKF), Jacob ‘Ghost’ Mulee amesema aliwahi kucheza kikosi kimoja
na Kisaka na alikuwa na uwezo mkubwa sana.
“Namkumbuka sana Kisaka, alikuwa na
uwezo wa juu akiwa langoni wakati tukicheza pamoja katika timu ya Volcano,”
alisema.
“Unajua mimi nilikuwa kipa
ninayechipukia na Kisaka hakuwa mchoyo kwa mafunzo, namkumbuka sana.”
Mulee pia amewahi kuwa kocha wa Kenya,
Harambee Stars na kupata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kuchukua Kombe la
Chalenji.
0 COMMENTS:
Post a Comment