Kocha wa zamani wa Simba, Patrick
Liewig amesema uvumilivu umekwisha kwake.
Amesema amekuwa akipewa ahadi kila
siku na Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage.
Liewig amesema Rage kila mara amekuwa
akimuahidi kukutana naye bila ya mafanikio kwa madai yuko busy.
“Kweli najua yuko busy, lakini vizuri
atekeleze ahadi zake anazonipa, sipendi kulumbana na watu wa Simba.
“Nimekuwa muungwana na mvumilivu
lakini sasa nimechoka kuhusiana na suala hili na hasa mwenyekiti, kweli
ananiumiza sana na ajue nimetoka mbali kuja hapa kwa ajili ya
walichoniahidi,”
alisema Liewig raia wa Ufaransa.
Jana alisema, Simba waliahidi kumlipa
dola 10,000 kati ya 16,000 anazowadai lakini hawakutekeleza ahadi.
Badala yake wakamlipa dola 7,000
kabla ya kuongeza dola 1000 na kuwa 8000.
“Sasa nawadai dola 8,850 ambazo
wanatakiwa wanilipe fedha zangu zilizobaki, tayari nimeanza kuwa na hofu,”
alisema Liewig.
0 COMMENTS:
Post a Comment