Real Madrid imetoa sare ya mabao 2-2
ikiwa ugenini dhidi ya Juventus na Cristiano Ronaldo na Bale, kila mmoja
akifunga bao moja.
Katika mechi hiyo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Juventus
walipata mabao yao mawili kupitia Vidal kwa mkwaju wa penalti na Llolente kwa
kichwa.
Manchester City wao wakafanya kweli
kwa kushinda mabao 5-2 dhidi ya CSKA Moscow huku Kun Aguero akipiga mbili na Nagredo
akipiga hat trick.
Mechi nyingine FC Kopenhagen
ikaichapa Galatasaray bao 1-0, Shaktar ikatoka sare ya bila kufungana na Beyer
Leverkusen sawa na Manchester United ikabanwa na Real Sociedad ikiwa ugenini.
Mabingwa Bayern Munich wao kwa tabu
wakiwa ugenini wameshinda kwa bao 1-0 dhidi ya Viktoria Plzen mfungaji akiwa ni
Mandzukic.
Zlatan Ibrahimovic naye akaendelea kuonyesha ubora wake baada ya kuisaidia PSG kupata sare ya bao 1-1 baada ya kufunga bao lakini wageni Anderlecht ya Ubeligiji wakawa wabishi na kusawazisha.
.
.
0 COMMENTS:
Post a Comment