November 28, 2013





Mlezi wa Simba, Rahma Al Kharusi amefunguka na kusema ndani ya klabu hiyo kumekuwa na matatizo mengi kwa kipindi kirefu.


Rahma maarufu kama Malkia wa nyuki, amesema Simba ina nafasi kubwa ya kuendelea lakini kutoelewana kati ya Mwenyekiti, Ismail Aden Rage na viongozi wenzake kumekuwa ni tatizo kubwa na pande zote mbili zinasababisha mgawanyiko.

Akizungumza katika mahojiano maalum jana, Malkia wa nyuki amesema kila upande unaweza kuwa na sehemu ya kuchota lawama ingawa sasa si kipindi mwafaka cha kufanya hivyo.


“Kama nilivyosema awali, mimi sina upande ndani ya Simba, siko kwa Rage wala kamati ya utendaji. Upande wowote naweza kushirikiana nao kama unalenda kuleta maendeleo kwenye klabu.

“Lakini kila upande, ninamaanisha mwenyekiti (Rage) hata baadhi ya wajumbe wa kamati ya utendaji nao ni matatizo na si ya leo tu, yamekuwa yakikua taratibu hadi leo yamefikia hapa.

“ Kuna mambo mengi yanaonyesha ubinafsi wao, wengine wanahofia wengine kupata sifa, vizuri kama wangetanguliza maendeleo ya klabu kwanza, sifa baadae.

“Wako watu wanafanya kazi kwenye klabu kwa ajili ya maslahi yao binafsi, hawataki kuona mambo yanakwenda haraka na hasa kama wakiona hawafaidiki.

“Mimi ni msemakweli na wala sina hofu. Kikubwa hapa ni kumaliza matatizo ya sasa ili tuendelee mbele kwa ajili ya kuwatumikia Wanasimba na kuleta maendeleo.

“Inawezekana kuleta maendeleo, lakini kama watu watakuwa wabinafsi basi hakutakuwa na maendeleo yatakayopatikana. Sitaki kusema mambo mengi sana zaidi ya hapa,” alisema Malkia wa nyuki.

Malkia wa nyuki sasa ni mmoja wa wajumbe wa bodi ya wadhamini wa Simba, cheo ambacho amepewa na Rage aliyekuwa tayari ametangazwa kusimamishwa lakini mwenyewe akapinga kuhusiana na hilo na kusema walikiuka katiba.
Lakini baadhi ya wachambuzi wa mambo wanaeleza kuwa Rage ameamua kumuondoa ndani ya kamati ya utendaji ili apate nafasi nzuri ya kupambana na waliobaki.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic