Mashabiki wa Yanga na Simba
wameendelea kutesa kupitia kampeni za Nani Mtani Jembe zilizofanyika mkoani
Dodoma.
Katika Bonanza lililofanyika
mjini humo, mashabiki hao walishindana katika michezo mbalimbali ikiwemo soka.
Mbali na soka uwanjani,
mashabiki wa Simba na Yanga walionyeshana kazi katika upigaji wa kontroo huku
wakishangiliwa kwa nguvu.
Baada ya tamasha hilo,
mashabiki wa Yanga na Simba waliipongeza bia ya Kilimanjaro ambao ni wadhamini wa
Simba na Yanga na walioandaa bonanza hilo na kutaka liendelee kufanyika zaidi
ya mara moja.
Walisema liliwachangamsha na
imeonyesha kiasi gani Kilimanjaro Premium Lager wanavyowajali Watanzania.
0 COMMENTS:
Post a Comment