Palikuwa
hapatoshi katika viwanja vya burudani vya Leaders Club jijini Dar es Salaam
pale wasanii mahiri mapacha Peter na Paul Okoye alimaarufu kama P Square kutoka
nchini Nigeria walipozikonga vilivyo nyoyo za mashabiki kwa takribani muda wa
masaa matatu mfululizo jukwaani.
Tamasha
hilo ambalo lilifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita ya Jumamosi 23 Novemba,
ilikuwa haijawahi kutokea nchini kwani mashabiki wamekiri uwezo wa kutumbuiza
jukwaani pamoja na kutumia ala mbalimbali za muziki na wasanii hao ni wa hali
ya juu.
Tamasha
lilikuwa lenye kuburudisha sana kwani usalama ulikuwepo wa kutosha kitu ambacho
wengi tulikifurahia, alisema bwana Rajabu Abdallah, mmoja wa mashabiki
waliohudhuria usiku huo.
“Pongezi
zangu za dhati nazielekeza kwa wadhamini wa tamasha hilo,Vodacom Tanzania,kwa
kufanikisha ujio wa wasanii hawa na kubuni njia mbadala ya M-PESA kwa mashabiki
kuweza kukata tiketi bila usumbufu wowote”kwa raha zetu”siyo kama miaka ya
nyuma foleni na adha za wizi kwenye foleni ungetokea.Nawaomba wasife moyo
waendelee kufanya hivyo kwani sio tu, wanatoa burudani kwetu mashabiki wa
muziki bali wanawapa fursa wasanii wetu kujifunza kutoka kwa wenzetu wenye
uzoefu wa kimataifa na pia sifa kwa nchi yetu kwani dunia nzima ilikuwa
ikifahamu P Square wanafanya tamasha kubwa la muziki nchini.” Aliongeza
Abdallah.
Rashid
Nassoro alikuwa pia ni mmojawapo wa mashabiki waliokuwepo kwenye viwanja hivyo
ambapo amesifia usalama wa hali ya juu uliokuwepo ndani na nje ya tamasha kwani
hakukuwa na malalamiko ya aina yoyote ya mtu kufanyiwa kitendo chochote cha
uhalifu.
“Mara
nyingi tumekuwa na hofu ya vibaka ambao wamekuwa wakitishia usalama wetu kiasi
kwamba tumekuwa tukiacha vitu vyetu vya gharama kama vile simu na fedha
nyumbani kwa kuhofia kuibiwa na hivyo kupunguza idadi ya wengi kuja
kuhofia usalama wao na mali zao. Lakini katika tamasha hili hali imekuwa ni
kinyume na tulivyotarajia kwani mashabiki na wakazi wa maeneo ya karibu
wameonesha ustaarabu na ukomavu wa juu katika kuelewa ni nini maana ya watu
kujumuika na kufurahi kwa pamoja bila la uvunjifu wa amani, alimalizia
Nassoro.
Wakati
huohuo, Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Kelvin
Twisa amesema kwamba wao kama wadhamini wa tamasha hilo nchini wamefurahishwa
na ushirikiano waliouonesha kufanikiwa kwa tukio hilo la kihistoria katika
tasnia ya burudani nchini.
“Tamasha
hilo limekuwa lenye mafanikio kwetu kwani hali ya utulivu iliyojitokeza siku
ile ni dhahiri kwamba watanzania sasa wanaelewa nini maana ya burudani, na hii
inazidi kutupa moyo wa kuzidi kudhamini matamasha mengi kadri tuwezavyo na
tunaahidi kufanya hivyo.”
Wingi
wa mashabiki waliojitokeza siku ile inaonesha ni jinsi gani tunakubalika na
kuungwa mkono, Vodacom siku zote utabaki kuwa mtandao unaowajali wateja wake
katika Nyanja zote na si huduma na bidhaa wanazozitoa, kwa niaba ya kampuni
ningependa kuwashukuru sana Serikali kwa kuweka usalama wa hali ya juu,Pia na
watanzania kwa kujitokeza kwa wingi kwa ustaarabu mliouonesha siku ya tukio, na
hilo imedhihirisha kweli nchi yetu ni kisiwa cha amani na utulivu.” Alimalizia
Twisa.
Mbali
na P Square katika tamasha hilo, pia wasanii nguli wa bongo flava Profesa Jay,
Lady Jay Dee, Ben Pol pamoja na Joh Makini walidhihirisha kwa umati wa
mashabiki waliokuwepo viwanjani hapo kwamba kiingilio chao hakikuenda bure.
Wasanii hao waliipeperusha vilivyo bendera ya muziki wa Tanzania kwa wakali hao
wa Nigeria kwamba hata sisi tunaweza kufanya makubwa tuwapo jukwaani.
0 COMMENTS:
Post a Comment