AMROUCHE |
Mechi ya kirafiki kati ya Taifa Stars
dhidi ya Harambee Stars iliyopangwa kuchezwa kesho imeyeyuka.
Kocha Mkuu wa Kenya, Adel Amrouche
amethibitisha kuwa mechi hiyo kesho haitakuwepo.
“Kweli hakutakuwa na mechi na
matatizo yametokea hapa Kenya, wachezaji hawakupatikana kwa wakati unaotakiwa.
“Waambie mashabiki wa Tanzania
nimesikitika kutokuja kucheza,” alisema.
“Nawaheshimu na mashabiki wa soka wa
Tanzania ambao wamekuwa wakijitokeza kwa wingi kuishangilia timu yao. Huenda siku
nyingine tutakuja na kucheza hapo.”
Mechi hiyo ilipangwa kuchezwa kesho
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.
0 COMMENTS:
Post a Comment