Beki mkongwe, Rio
Ferdnand ame twitt na kueleza walivyonusurika na ajali ya ndege jana wakati
wakitua Ujerumani kuivaa Bayer Leverkusen katika Ligi ya mabingwa leo.
Kikosi
cha Manchester United kinachoongozwa na Kocha David Moyes kimenusurika na ajali
ya ndege nchini Ujerumani.
Wakati
ndege iliyowabeba Manchester United ikitua kwenye uwanja wa ndege we Cologne,
mara rubani aligundua kuna ndege nyingine waliyokuwa wanakwenda kuigonga.
Haraka
aliinua juu tena ili kuikwepa iliyokuwa chini na kwenda kutua mbele ya eneo
walilotakiwa kutua mbele.
Kutokana
na kasi hiyo wachezaji na maofisa wengine waliokuwa kwenye ndege hiyo
walianguka kwenye viti.
Hali
hiyo ilisababisha hofu kubwa ndani ya ndege hiyo, baada ya kutua rubani pamoja
na uongozi wa shirika hilo la ndege uliomba radhi.
Manchester
iliwahi kupata ajali ya ndege mwaka 1958 na kusababisha vifo vya wachezaji
kadhaa.
0 COMMENTS:
Post a Comment