Mathieu
Flamini ameingia kwenye mgogoro na Kocha Arsene Wenger kutokana na kitendo
chake cha kukata mikono ya jezi.
Kiungo
huyo ameonyesha kutovutiwa na jezi ya mikono mirefu hivyo amekuwa akizikata
mikono kwa makusudi.
Lakini
Wenger amesisitiza kwamba hatamruhusu kucheza iwapo atafanya hivyo kwa mara
nyingine.
Awali
hakuwa amejua kuwa Flamini anafanya hivyo hadi aliposimuliwa na mtunza vifaa
alionyesha kukasirika na kumtaka Flamini kufuata utamaduni we Arsenal kama
wachezaji wote wanavaa jezi za mikono mirefu basi ni wote.
Kwa
timu nyingine, wachezaji huruhusiwa kuchagua jezi za mikono mirefu au mifupi.
0 COMMENTS:
Post a Comment