November 15, 2013





Washambuliaji wawili wa Tanzania, Taifa Stars, Mbwana Samatta na Mrisho Ngassa ndiyo tishio zaidi kwa kikosi cha Kenya, Harambee Stars.


Stars itaikaribisha Harambee, Jumanne ijayo katika mechi ya kirafiki itakayopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Kocha Mkuu wa Harambee Stars, Adel Amrouche ambaye anasifika kwa soka la mipango, amesema Samatta na Ngassa wanapaswa kulindwa vema.

“Unapokutana na kila timu lazima uangalie uimara wa wapinzani wako uko wapi na kipi cha kufanya. Siwezi kukataa kuhusiana na ubora wa Samatta, pia Ngassa. Najua mengi sana kuhusu Tanzania lakini ni suala la kulifanyia kazi,” alisema Amrouche, raia wa Ubelgiji na kuongeza:

“Pia ninajua kuna Thomas (Ulimwengu) na wengine, hivyo ni kazi ngumu ambayo inahitaji hesabu. Kweli ni mechi ya kirafiki lakini najua kila upande utataka kushinda.”

Tayari wachezaji wa kimataifa wa Kenya wapo jijini Nairobi, akiwemo Victor Wanyama anayekipiga Southampton ya England na Denis Oliech anayeitumikia Ajaccio ya Ufaransa.

Nyota mwingine wa Harambee ni kiungo wa Inter Milan, McDonald Mariga anayekipiga Parma kwa mkopo, hajaitwa katika kikosi hicho cha Amrouche maana hakuwa fiti lakini kiungo Mohammed Jamal anayekipiga nchini Oman tayari yupo Nairobi kujiandaa na mechi hiyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic