November 5, 2013




Kocha Patrick Liewig amesema uongozi wa Simba umemlika dola 7,000.


Liewig raia wa Ufaransa ambaye anadai dola 16,000 amesema amelipwa dola 7,000 na si 10,000 kama ambavyo imekuwa ikielezwa.

“Nimelipwa dola 7,000 leo mchana, lakini wameniahidi wanaendelea kukusanya na watanilipa nyingine 3,000.
“Naendelea kusubiri kwa kuwa ahadi ilikuwa walipe dola 10,000 na nyingine 6,000 watanilipa siku nyingine kulingana na makubaliano.

“Niko hapa ila siwezi kusema ni wapi naendelea kusubiri waje kunilipa kiasi kilichobaki. Baada ya hapo nitaondoka,” alisema.

Awali Simba ilimlipa Liewig dola 10,000 kati ya dola 26,000 alizokuwa anadai klabu hiyo baada ya kumvunjia mkataba na kuahidi kumlipa kiasi kilichobaki mwezi uliopita.

Liewig alikuwa anadai malimbikizo ya mishahara ya miezi miwili, dola 12,000 na dola 12,000 za kuvunjiwa Mkataba wakati dola 2,000 ni za tiketi yake ya kurejea kwake.
Liewig alichukua nafasi ya Milovan Cirkovic na baada ya nusu msimu naye akatupiwa virago na nafasi kwenda kwa Abdallah Kibadeni.

1 COMMENTS:

  1. huu ubabaishaji simba utaisha lini, rage juzi tu umechukua million 300 utoka azam TV embu mlipe lewing mbaki na makocha wenu kina kibadeni wa uswahilini,...inakera sana

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic