AWADHI JUMA (KULIA) WAKATI AKIWA MTIBWA SUGAR AKIWA JUMA ABDUL WA YANGA MIEZI MICHACHE ILIYOPITA BAADA YA MECHI YA LIGI KUU BARA MZUNGUKO WA KWANZA KWENYE UWANJA WA TAIFA. |
Simba ambayo bado haijakaa vizuri kwenye Ligi Kuu
Bara, leo imefanikiwa kuongeza nguvu kwa kusaini wachezaji wawili, Awadh Juma
Issa na Ally Badru Ally.
Issa ni kiungo aliyekuwa anakipiga Mtibwa Sugar wakati
Badru ni mshambuliaji aliyewahi kukipiga nchini Misri katika timu ya Canal Suez iliyokuwa inashiriki ligi daraja la kwanza hadi ilipopanda ligi kuu msimu huu, ingawa hakufanikiwa kucheza hata mechi moja.
Wawili hao wote ni wachezaji walio katika kikosi cha
Zanzibar Heroes kitakachoshiriki michuano ya Chalenji nchini Kenya kuanzia
Novemba 27.
Mara baada ya kutua jijini Dar na kusaini mkataba huo
nyumbani kwa Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage waliondoka na kurejea
Zanzibar.
Awali Simba ilikuwa ikifanya mchakato wa kupata kiungo na
Hassan Saleh Dilunga alikuwa kwenye target zao kabla ya Yanga kumyakua njiani.
0 COMMENTS:
Post a Comment