November 18, 2013


Mpachika mabao wa Simba, Amissi Tambwe, amesema timu yao inahitaji kuongeza kiungo na winga mmoja kwenye usajili wa dirisha dogo.


Usajili huo wa dirisha dogo ulifunguliwa Ijumaa iliyopita na unatarajiwa kufungwa Desemba 15, mwaka huu.

Tambwe amesema nafasi hizo ndizo zenye upungufu na kwamba ndizo zilizosababisha kushindwa kutimiza idadi ya mabao aliyopanga katika mzunguko wa kwanza wa ligi.

Tambwe alisema katika mzunguko wa kwanza, amefunga bao moja pekee la kichwa kutokana na timu yao kukosa winga mwenye uwezo wa kupiga krosi nzuri za kufunga.

“Ujue katika mabao yangu kumi niliyofunga kwenye mzunguko wa kwanza wa ligi, yote nilifunga kwa mguu, kwa njia ya pasi, isipokuwa moja pekee nililofunga kwa kichwa.

“Nimeshindwa kufunga kwa kichwa kutokana na timu kukosa mawinga wenye uwezo wa kupiga krosi, hivyo ili niendelee kufunga mabao kwenye mzunguko wa pili wa ligi, basi viongozi wasajili winga na kiungo mwenye uwezo,” alisema Tambwe.

Mshambuliaji huyo anaongoza kwa mabao kwenye ligi kuu akiwa na 10, akifuatiwa na Elius Maguri wa Ruvu Shooting aliyefunga 9 na Hamis Kiiza wa Yanga mwenye 8.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic