Na Boniface Wambura
Wakati
dirisha dogo la usajili linafungwa Desemba 15 mwaka huu, Shirikisho la Mpira wa
Miguu Tanzania (TFF) tunazikumbusha klabu zote kuheshimu kanuni na kuzingatia
muda uliowekwa.
Pia tunakumbusha kuwa kupeleka
mchezaji kwa mkopo katika klabu nyingine hakutoi nafasi ya kusajili mchezaji
mpya. Kama klabu ilisaji wachezaji 30 maana yake ni kuwa haina nafasi ya
kuongeza wachezaji.
Kwa upande wa wachezaji wa
kigeni (foreign players), tunakumbusha kuwa kuanzia msimu ujao 2014/2015
watakuwa watatu tu badala ya watano wa sasa.
Kuhusu usajili wa wachezaji
kutoka nje mpaka sasa hakuna hata klabu moja imeshaingia kwenye TMS kuomba
uhamisho. Itakapofika Desemba 15, system ya TMS itafunga.
0 COMMENTS:
Post a Comment