Arsenal imezidi kupaa katika Ligi ya Mabingwa Ulaya
baada ya kuichapa Marseille kwa mabao 2-0.
Mabao yote ya Arsenal yamefungwa na Jack Wilshere
ambaye aling’ara katika mechi hiyo kwenye Uwanja wa Emirates mjini London.
Katika mechi nyingine, Mohammed Salah wa Basle
akaendeleza ubabe wake kwa Chelsea kwa kufunga bao pekee na kikosi cha Jose
Mourinho kikalala kwa bao 1-0.
Wababe wengine Barcelona wakiwa ugenini wakakumbana
na kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Ajax.
AC Milan nao wakazinduka kwa ushindi we mabao 3-0
wakiwa ugenini dhidi ya Celtic na Balotelli na Kaka kila mmoja akitupia bao moja.
Borussia Dortmund waliofungwa na Arsenal waliofungwa
na Arsenal mechi iliyopita wakaamka na kuichapa Napoli kwa mabao 3-1.
Schalke wakiwa ugenini wakalazimisha sare ya bila kufungana
dhidi ya Steau Bucharest, Zenit nao wakalazimishwa sare ya 1-1 na wageni wao
Atletico Madrid huku FC Porto waliokuwa nyumbani wakafanya kazi ya ziada pia
kupata sare ya bao 1-1.
0 COMMENTS:
Post a Comment