Aliyekuwa kocha mkuu wa Tanzania
Prisons, Jumanne Chale ameibuka na kusema kuwa ameamua kuachana na soka kwa
sasa na badala yake amegeukia biashara zake mpaka hapo baadaye.
Chale alitimuliwa Prisons kabla ya
msimu huu kufikia katikati kufuatia timu hiyo kufanya vibaya katika mechi zake
kadhaa za mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Bara.
Chale
amesema kwa sasa hafikirii masuala ya mpira na amepumzika kwa kuanzisha biashara
zake na mambo mengine madogo-madogo.
“Kwa sasa nipo nyumbani nimepumzika na
wala sifikirii suala la soka labda hadi msimu utakapoisha ndipo nifikirie
kujiunga na timu nyingine. Kwa sasa nafanya biashara zangu na mambo mengine ya
kimaisha,” alisema Chale.
SOURCE: CHAMPIONI
0 COMMENTS:
Post a Comment