November 21, 2013





Baraza la wadhamini la Simba limesema linaendelea kumtambua Ismail Aden Rage kama mwenyekiti.

Rage bado yuko nchini Sudan na anatarajia kurejea kesho nchini na moja kwa moja atazungumza na waandishi wa habari.


Lakini mmoja wajumbe wa Baraza hilo, Hamis Kilomoni ameonekana kujikanyaka kujibu maswali kuhusiana na uamuzi wao.
MZEE KILOMONI

Hata hivyo baraza hilo lilikutana na wajumbe wawili tu ambao ni Kilomoni na mwenzake Ramesh Patel
SALEHJEMBE: Labda mnahisi kamati utendaji imekosea katika kumsimamisha?
KILOMONI: Ndiyo maana hawajafuata katiba.
SALEHJEMBE: Labda kipengele kipi unaweza kufafanua?
KILOMONI: Aaah, hadi nisome? Ila lengo letu ni kusuluhisha hili jambo.
SALEHJEMBE: Kama ni kusuluhisha vipi tayari mmeingia na maamuzi yenu tayari kwamba mnamtambua Rage ni mwenyekiti.
KILOMONI: Kweli shida yetu ni kuwakutanisha pande zote hizi mbili baada ya Rage kufika kesho (Ijumaa jioni).
SALEHJEMBE: Katiba inawaruhusu kuingilia masuala ya kiutendaji?
KILOMONI: Hapana haituruhusu lakini sisi pia ni wazee na kama tuna tatizo unataka tuliache tu?
SALEHJEMBE: kweli hamsitahili kuliacha, lakini sasa Simba haina baraza la wazee, sasa nyie mnasimama upande upi?
KILOMONI: Kweli hatuna baraza na litaundwa hivi karibuni, lakini bado sisi ni wazee. Tunaenda kama wazee.
SALEHJEMBE: Naona kama unajichanganya Mzee Kilomoni, mara kama wadhamini mara kama wazee, kipi hasa sahihi na vipi mmetengua uamuzi wa kamati ya utendaji.
KILOMONI: Nimekuambia wamejiuka katiba.
SALEHJEMBE: Sawa, lakini ibara au kipengele kipi?
KILOMONI: Nimesema nimesahau hadi nijisomee tena, au nenda katafute mwenye katiba ya Simba. Kwaheri.
SALEHJEMBE: eeh!

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic