Kikao kilichopangwa kufanyika kwenye
makao makuu ya Simba kimekwama baada ya Kaimu mwenyekiti wa klabu hiyo, Joseph
Itang’are ‘Mzee Kinesi’ kuingia uoga.
Mzee Kinesi ameingia uoga na kushindwa
kufanya kikao hicho na waandishi walikuwa kibao wakimsubiri.
“Mzee Kinesi alisema amekwama kwenye
foleni,” alieleza mwandishi wa gazeti moja.
Hata hivyo haikujulikana Mzee Kinesi alikuwa anataka kuzungumza kitu gani.
Lakini taarifa za uhakika zilieleza
kwamba Mzee Kinesi alihofia wanachama kibao waliojitokeza klabuni hapo.
“Mzee Kinesi kawaambia waandishi waende
kikao kikafanyike kwa mmoja wa wazee wa baraza la wazee, Mzee Kilomoni,”
alisema mwandishi mwingine wa runinga.
Tayari kikao hicho cha waandishi
kimeanza nyumbani kwa Mzee Kilomoni jijini Dar.
0 COMMENTS:
Post a Comment