Watanzania watatu wameombewa Hati ya Uhamisho wa
Kimataifa (ITC) na Chama cha Mpira wa Miguu Ujerumani (DFB) ili wacheze mpira
wa miguu nchini humo.
Wachezaji hao ni Charles Mishetto na David Sondo
wanaombewa hati hiyo ili waweze kujiunga na timu ya SpVgg 1914 Selbitz, wakati
Eric Magesa ameombewa kibali hicho ili achezee timu ya klabu ya SC Morslingen.
Hata hivyo, katika maombi hayo DFB haikuleza hapa
nchini walikuwa wakicheza katika klabu zipi. Wachezaji wote wameombewa hati
hiyo kama wachezaji wa ridhaa.
0 COMMENTS:
Post a Comment