Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (Caf) limemteua
Lina Kessy kuwa kamishna wa mechi ya Kombe la Dunia Kanda ya Afrika kwa
wanawake chini ya umri wa miaka 20 kati ya Afrika Kusini na Botswana.
Mechi hiyo ya marudiano ya raundi ya kwanza itachezwa
nchini Afrika Kusini, Novemba 9 mwaka huu. Waamuzi kutoka Zambia ndiyo
watakaochezesha mechi hiyo namba kumi.
Waamuzi hao wataongozwa na Glads
lengwe atakayepuliza filimbi wakati mwamuzi msaidizi namba moja ni Bernadette
Kwimbira kutoka Malawi, namba mbili ni Mercy Zulu na mezani atakuwepo Sarah
Ramadhani, wote wa Zambia.
Afrika Kusini ilishinda mechi ya
kwanza ugenini mabao 5-2. Mshindi wa mechi hiyo atacheza raundi ya pili na
mshindi wa mechi kati ya Tanzania na Msumbiji.
0 COMMENTS:
Post a Comment