Uongozi wa Kagera Sugar, umethibitisha
kuwa katika hatua za mwisho kumalizana na aliyekuwa beki wa kati wa Yanga,
Chacha Marwa, ambaye kwa sasa anakipiga kwenye klabu ya Ligi Daraja la Kwanza,
Ndanda FC ya Mtwara.
Kagera imekuwa ikihaha kumpata beki wa
kati mwenye uzoefu mkubwa tangu kuumia kwa Amandus Nesta msimu uliopita.
Mrage Kabange,
alisema: “Kila kitu kimekamilika kwa upande wa timu, tumebakiza makubaliano
yetu na mchezaji mwenyewe, japo tayari tumeteta naye, sema hatujamalizana
kwenye kipengele cha maslahi. Naamini kufikia Desemba 10 (kesho), kila kitu
kitakuwa wazi.”
Kagera Sugar ni moja ya timu ambazo
zimekuwa zikitoa ushindani wa kutosha kwenye Ligi Kuu Bara na katika mzunguko
wa kwanza imemaliza ikiwa kwenye nafasi ya tano, ikiwa na pointi 20 ambazo ni
nane pungufu ya vinara, Yanga.







0 COMMENTS:
Post a Comment