Kipa
Juma Kaseja amekiri kukutana na ugumu wa mazoezi ya timu Yanga chini ya kocha wa
makipa, Razack Siwa.
Kaseja ametoa kauli hiyo Alhamisi
iliyopita mara baada ya kumalizika kwa mazoezi kwenye Uwanja wa Bora,
Kijitonyama jijini Dar es Salaam.
Kaseja amesema kuwa tangu ajiunge Yanga, amekuwa akikutana na mazoezi magumu
ambayo ameshindwa kuyatofautisha na yale ya Simba.
Kaseja alisema anayafurahia mazoezi
hayo, akiamini yatamjenga katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
“Nimefanya mazoezi na Yanga kwa siku
nne, ni ngumu kutofautisha ya hapa na nilipotoka Simba, lakini tambua kwamba
mazoezi niliyoyakuta Yanga ni magumu.
“Licha na ugumu huo, nitajitahidi
kuyafanya kwa ajili ya kunijenga katika mzunguko wa pili wa ligi ili niongeze
kiwango changu,” alisema Kaseja.







0 COMMENTS:
Post a Comment