Kipa Juma Kaseja leo ameanza rasmi
kuitumikia Yanga ambayo ameingia nayo mkataba wa miaka miwili.
Kaseja ameanza mazoezi leo kwenye Uwanja
wa Bora Kijitonyama jijini Dar es Salaam na kuwa kivutio kwa wengi
waliohudhuria mazoezi hayo.
Kipa huyo wa zamani wa Simba, amekutana
na Ally Mustapha ‘Barthez’ aliyekuwa kipa msaidizi wake walipokuwa Simba.
Wakati fulani Barthez aliwahi kulalamika
kwamba hakuwa akipata nafasi ya kudaka kwa kuwa Kaseja alikuwa akidaka mechi
zote.
Lakini Mungu si Athumani! Makipa hao
wamekutana kwa mara nyingine, wakiwa nje ya mipaka ya Msimbazi, safari hii
Msimbazi.
0 COMMENTS:
Post a Comment