December 30, 2013




Siku chache baada ya Kocha Mkuu wa Ruvu Shootings, Charles Mkwasa, kuweka wazi kuwa amemalizana na uongozi wa klabu hiyo kutaka kuondoka, tayari Ruvu wamepanga kumtangaza rasmi mrithi wake keshokutwa Alhamisi, ambaye atakiongoza kikosi hicho katika raundi ya pili ya ligi kuu.
 
Mkwasa  amekubali kufanya kazi na mabingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Yanga SC, kama kocha msaidizi huku akichukua mikoba ya Fred Felix ‘Minziro’ ambaye hatima yake mpaka sasa haijajulikana huku kocha mkuu Ernie Brandts akitimuliwa kazi kutokana na mwenendo mbaya wa timu.
Msemaji wa Ruvu, Masau Bwire, alikiri kuwa Mkwasa amefikisha barua kwa viongozi wake  hivyo wanahaha kumtafuta mrithi wake haraka iwezekanavyo.
“Ni kweli Mkwasa, ameonesha nia ya kuondoka, tumemshauri kubaki lakini hakutaka na tayari amewasilisha barua ya kuondoka. Kuhusu mrithi wake atatangazwa rasmi Januari 2, siku ambayo tutaweka bayana kila kitu, likiwemo la mkataba wake,” alisema Bwire.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic