Timu ya
Bara, Kilimanjaro Stars imepata ushindi wake wa kwanza katika michuano ya
Chalenji kwenye Uwanja wa Nyayo jijini Nairobi, Kenya.
Bao pekee
katika mcheoz huo lilifungwa na Haruna Chanongo katika kipindi cha pili
akiunganisha krosi safi ya Frank Domayo aliyekuwa amepewa pasi ya chini ya Ramadhani
Singano ‘Messi’.
Pamoja na Stars kujitahidi na kulishambulia mfululizo
lango la Somalia lakini bado washambuliaji wake hawakuwa makini katika kufunga.
Katika
mechi ya kwanza Stars ilitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Zambia katika uwanja wa
Machakos uliokuwa umejaa tope kama wa mchangani.
0 COMMENTS:
Post a Comment