December 20, 2013





Kipa namba moja wa Mbeya City, David Burhan amesema kuvaa jezi namba 18 kwake kuna maana kubwa hasa katika maisha yake.


Mbeya City ilimsajili kipa huyo msimu huu akitokea Tanzania Prisons ambapo ameliambia gazeti hili kuwa, namba 18 inawakilisha siku yake ya kuzaliwa na siyo jambo lingine lolote na kusisitiza kuwa, ndiyo maana imekuwa yenye bahati kwake.

“Wengi wananiuliza kwa nini sikuchagua jezi namba moja kwa kuwa mimi ni kipa, lakini hii ni kawaida yangu kuitumia namba hiyo.

“Hata kwenye timu zangu za awali kabla ya kutua Mbeya City nilikuwa nikiitumia namba hiyohiyo, ikitokea naenda sehemu nyingine nitavaa namba hiyo pia. Nilipokuwa Polisi Iringa na Prisons kote nilivaa namba 18,” alisema Burhan.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic