December 20, 2013




Baadhi ya wachezaji wa Mtibwa Sugar wamegomea kujiunga na wenzao mazoezini kwa madai ya kutolipwa mshahara wa mwezi uliopita pamoja na wengine kutaka kuongezewa mikataba.


Kikizungumza na SALEHJEMBE, chanzo cha ndani kilisema wachezaji wengi mastaa wamegomea kwa kuwa hawajalipwa mshahara wa mwezi uliopita huku wengine wakiwa wamebakisha muda mchache kwenye mkataba wao, hivyo wanataka kuongezewa.

“Wamegomea kuanza mazoezi na wenzao, kuna madai mawili, mshahara wa mwezi uliopita pamoja na wengine ambao mikataba yao inakaribia kumalizika wanataka wapewe mipya,” kilisema chanzo hicho.

Alipotafutwa Meneja wa Mtibwa, David Gboya, alisema: “Mshahara tunaodaiwa ni wa mwezi huu ambao hata muda wa kulipa bado, ndiyo maana hawajaja, naona wanataka fedha za kuziachia familia zao, wao watakapokuwa kazini, wasijali kwa hilo.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic