December 25, 2013



 
WAKATI WA UHAI WAKE; KISAKA AKISAIDIWA KUVISHWA VIATU NA MWANAYE, HUKU AKIWA AMESHIKWA NA MKEWE MDOGO KWA KUWA HAKUWA AKIWEZA KUTEMBEA MWENYEWE.
Kocha wa zamani wa makipa wa Simba, James Kisaka ataangwa kesho Saa 9 Alasiri kabla ya kusafiriswa kwao Tanga kwa mazishi.
Kisaka aliyefariki leo alfajiri katika Hospitali ya Burhan, mwili wake utaangwa katika hospitali ya Muhimbili jijini Dar.
 
Kisaka alikuwa amepooza upande mmoja, ameugua kwa zaidi ya mwezi mmoja hadi alipolazwa katika hospitali hiyo.
Msemaji wa Familia, Benny Kisaka amesema mwili wake utasafirishwa kijijini kwao mkoani Tanga kwa mazishi baada ya kuangwa jijini Dar.
"Kwa sasa msiba uko Mbezi, ni mbele ya Mbezi kwa Msuguri nje kidogo ya jiji la Dar," alisema Kisaka ambaye ni mmoja wa waandishi waandamizi wa michezo na burudani.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic