December 8, 2013



AMROUCHE AKIWA NA MOSES ODHIAMBO

Kocha Mkuu wa Kenya, Harambee Stars, Adel Amrouche amesema mechi ya nusu fainali ya Kombe la Chalenji kati ya kikosi chake itakuwa ngumu.

Amrouche raia wa Ubelgiji mwenye asili ya Algeria amesema mechi itakuwa ngumu sana na kila timu italazimika kufanya kazi ya ziada.
“Kazi ni ngumu sana katika mechi hiyo, tunawaheshimu Tanzania lakini tunachotaka ni kushinda nyumbani.

“Tunataka kufanya vizuri na kubakiza kombe nyumbani, mechi dhidi ya Taifa Stars haitakuwa lelemama,” alisema Amrouche.
Kocha huyo ni kati ya wale wanaopewa sifa kubwa kutokana na soka la pasi na kasi na pia anajulikana kwa kuwa na mipango ya ushindi.
Wakati akiwa Kocha wa timu ya taifa ya Burundi, aliiongoza timu hiyo kuvifunga vigogo kadhaa kama Misri na Ivory Coast.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic