Na Saleh
Ally
UKIFUATILIA
kwa umakini uchezaji wa Arsenal, utagundua kuimarika kwa kiasi kikubwa kwa
kiwango hasa katika kiungo.
Hali
hiyo imesababisha mashabiki wa Arsenal kusahau kabisa kuhusiana na Cesc
Fabregas ambaye waliamini kama angerejea basi tatizo la kiungo lingeisha.
Arsenal
ina mashabiki wengi duniani kote ikiwemo Tanzania, pamoja na mabadiliko hayo
imekuwa ni nadra sana wao kumtaja Aaron Ramsey ambaye ana miaka 22 tu, lakini
tayari ameonyesha kuwa ndiye tegemeo la kikosi hicho cha Arsene Wenger.
Raia
huyo wa Wales amekuwa katika kiwango cha juu msimu huu na ndiye anaaminika kuwa
kiungo mwenye kiwango cha juu zaidi katika kipindi hiki kwenye Premiership.
Ajabu
ni hivi, mashabiki wa Tanzania, England na kote duniani, wamekuwa
hawamzungumzii sana na badala yake amekuwa gumzo zaidi kwa wataalamu wa soka.
Gumzo
lake kwa wataalamu linatokana na uchezaji wake, hesabu za mambo yake, mabao
aliyofunga na pasi alizotoa.
Katika
mechi 15 za Ligi Kuu England alizocheza, Ramsey ametoa pasi tano zilizozaa
mabao, amepiga mashuti 38 yaliyolenga lango na kivutio zaidi ni mabao nane
aliyofunga.
Mabao
nane ni katika Premiership, lakini amekuwa pia akifanya vizuri zaidi na kufunga
zaidi ya mabao manne kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Ingawa
Premiership haijafika hata nusu msimu, tayari Ramsey kitakwimu amefanya kazi
mara mbili kuliko ilivyokuwa msimu mzima uliopita.
Wastani
wake wa kutoa pasi zilizofika ni 87.2% ambao ni wa juu zaidi na amefanikiwa
kuwapiku viungo nyota au walionunuliwa kwa bei mbaya kama Oscar, David Silva,
Shinji Kagawa, Marouane Fellaini na hata mkongwe, Mikel Arteta ambaye anapewa
sifa ya kumsaidia Ramsey.
Kufanya
vizuri kwa Ramsey katika kipindi hiki kunaonyesha uwezo mkubwa wa jicho la
Wenger katika vipaji. Wengi wamekuwa wakisahau kazi ya Mfaransa huyo anapokuwa
anakuza kipaji.
Lawama
nyingi huwa kwake, yakipatikana mafanikio anasahaulika na siku mchezaji akiuzwa
lawama nyingi zinaenda kwake.
Aliwahi
kutakiwa kuachana na kiungo huyo baada ya Cardiff ambayo alimpeleka kwa mkopo
kutaka kumnunua, akakataa. Ikatoa dau ikitaka kumnunua, akakataa pia na baadhi
ya viongozi wa klabu wakaona anakosea.
Leo,
alichokuwa anakitaka kinaanza kuonekana na aliwahi kueleza kwamba mchezaji mwenye
uwezo wa michezo mingine ni rahisi kuwa na mafanikio.
Ramsey
alikuwa mchezaji wa mchezo wa raga, maarufu kama rubgy, halafu akashiriki
katika riadha za kupeana vijiti katika timu ya shule kabla ya kuamua kujikita
kwenye soka.
Kiungo
cha Arsenal chenye ‘wabaya’ watatu, Ramsey, Arteta na Mathieu Flamini kimemaliza
maisha ya majonzi kwa mashabiki wa Arsenal.
Inawezekana
haukuwa ukifuatilia Arsenal inapokuwa inacheza, mechi inayofuata angalia vitu
hivi vitatu kutoka kwa Ramsey; kujaribu chochote bila ya woga (anawaudhi
mashabiki Arsenal), kuendesha vilivyo kiungo (anamfurahisha zaidi kocha), kutoa
pasi au kufunga mabao matata (anarudisha urafiki kwa mashabiki/kocha).
TAKWIMU
2013
MECHI MABAO
PASI MASHUTI
15 8 5 38









0 COMMENTS:
Post a Comment