December 11, 2013





Kocha Mkuu wa Simba, Zdravok Logarusic, amesema washambuliaji wa timu hiyo, akiwemo Betram Mwombeki, hawajamridhisha na kuagiza uongozi kumtafutia watu makini zaidi.
 
Logarusic maarufu kwa jina la Loga, amesema Mwombeki ni mshambuliaji mzuri wa wastani, ambapo kikubwa ambacho ameshindwa kukikubali ni jazba zake uwanjani na kutaka uongozi wa Wekundu hao kusaka mtu makini zaidi atakayesaidiana na Amissi Tambwe.
Loga ambaye ni beki wa zamani wa kushoto wa Croatia, amesema tayari kazi hiyo ameshawakabidhi viongozi wa Simba, ambapo amesisitiza kama aina hiyo ya mshambuliaji anayemtaka akipatikana, Wekundu hao watakuwa na safu kali ya ushambuliaji.

 “Nimefanya kazi ya kuwaangalia kwa makini washambuliaji waliofika mpaka sasa, kidogo huyu Betram (Mwombeki) anaonekana kuna kitu anacho, lakini tatizo moja alilonalo ni jazba akiwa uwanjani, sijajua ni mazoezini tu au hata kwenye mechi,” alisema Loga.
“Nimewaambia viongozi kwamba kama wataweza waniongezee mshambuliaji mmoja mzuri zaidi ya huyu, ambaye atashirikiana na Amissi (Tambwe), ambaye nimepata sifa zake kwamba ni mtu makini kwenye kutekeleza majukumu yake ya ufungaji, nataka ubingwa hapa,” alisema Loga.
SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic