Beki mpya wa Saraswot Youth Club ya
Nepal, Shadrack Nsajigwa, anaendelea na mazoezi ya timu hiyo huku akilalamikia
baridi kali inamsumbua.
Nsajigwa na wenzake Pius Kisambale na
Godfrey Bonny ‘Ndanje’, walitimkia nchini humo kwa ajili ya kwenda kucheza soka
la kulipwa.
Nsajigwa amesema kikwazo kwake nchini
huko ni baridi pekee ambayo ameahidi kupambana nayo.
Nsajigwa alisema tayari ameanza mazoezi
na timu hiyo wakijiandaa na ligi kuu ya nchini humo inayotarajiwa kuanza wiki
mbili zijazo.
“Huku ninaendelea vizuri, kikwazo kwangu
huku ni hali ya hewa ya baridi ambayo ni kali sana, lakini haitanizuia
kuendelea kubaki kupambana katika kutafuta maisha.
“Tumeanza mazoezi ya pamoja na wachezaji
wenzetu kujiandaa na ligi kuu, itakayoanza wiki mbili zijazo,” alisema Nsajigwa
aliyewahi kuwa nahodha wa Yanga.








0 COMMENTS:
Post a Comment