![]() |
| KOKE AKICHUANA NA MESSI |
Na Saleh Ally
Pamoja na
Ligi Kuu England kupewa sifa ya ugumu zaidi, lakini inaonekana kuna ligi ambazo
zina ufundi mwingi zaidi kuliko hiyo ya England.
Hispania
‘La Liga’ wamekuwa wakipewa sifa kubwa ya uchezaji na timu zao ndiyo zinaongoza
kwa umiliki wa mpira na pasi za burudani.
Mfano
Barcelona, ndiyo timu yenye uwezo mkubwa wa kumiliki mpira huku ikipanga
mashambulizi bila ya kuupoteza kwa kipindi kirefu zaidi.
Hata kama
mabao ni muhimu, lakini pasi za uhakika ni burudani ambayo huwavutia mashabiki
wengi wa soka duniani kote.
Kwa hapa
nyumbani, Simba ndiyo imekuwa ikipewa sifa ya timu inayopiga pasi nyingi na
fupifupi ingawa katika siku za karibuni inaonekana kupoteza sifa hiyo na kuwa
na kikosi ambacho hata mashabiki wake hawakiamini kama ilivyokuwa hapo awali.
Mabao ni
burudani ya uhakika, pasi zinavutia pia mashabiki wengi lakini pasi zinazozaa
mabao ndiyo kipenzi cha makocha wengi wa soka.
Kila kocha
anataka kuwa na mchezaji mwenye uwezo mkubwa wa kupiga pasi za mwisho zinazozaa
mabao na kuisaidia timu yake kuibuka na ushindi, maana timu ili ishinde lazima
ifunge na kuzuia kufungwa.
Ili ifunge,
lazima pasi ya kusababisha bao ipatikane. Hayo ni mafunzo na uwezo wa mchezaji
binafsi na inaonekana wachezaji wengi wa aina hivyo wanaishi Hispania
inapochezwa La Liga.
Wachezaji
hao wako La Liga bila ya kujali uraia wao ni nchi gani na katika takwimu za wapiga
pasi mahiri zilizotolewa wiki iliyopita, zinaonyesha wachezaji wengi
wanaokipiga katika ligi hiyo ya Hispania ndiyo wakali.
Wachezaji
kutoka England yaani Premiership wameachwa mbali na wakali kutoka Hispania na
hata wale wa Ujerumani, Bundesliga.
Ukichukua
tano bora ya Ulaya ya wapigaji bora wa pasi za mwisho, hukuti hata mchezaji
mmoja kutoka England. Kwani watatu wa juu wote wametoa pasi nane zilizozaa
mabao na wanatokea Hispania.
Wakali hao
wenye pasi nane ni Koke wa Atletico, Cesc Fabregas na Neymar (wote Barcelona).
Halafu wanafuatia wenye pasi sana ambao wote wanatokea Ujerumani ambao ni Gonzalo
Castro wa Bayer Leverkusen na mchezaji bora Ulaya, Frank Ribery wa
Bayern.
Hakuna mchezaji hata moja wa England aliyeingia katika
kikosi hicho cha tano bora cha kina ‘master’ wa kupiga pasi kwa kuwa mtu wa
kwanza kwa pasi za mabao England ni Steven Gerrard wa Liverpool.
Gerrard ana pasi sita sawa na Mesut Ozil wa Arsenal ambaye
alikuwa mchezaji wa Real Madrid kabla ya kutua mitaa ya Emirates msimu huu.
Wengine
wanaounda tano bora ya wapiga pasi England ni Wayne Rooney (Man United), Aaron Ramsey
(Arsenal) na Kevin
Mirallas wa Everton.
Ukiangalia
kwa England kwa kiasi kikubwa utaona kweli utoaji pasi za mwisho, zaidi
unategemea kipaji cha mchezaji husika.
Angalia Man
United, bado inayumba kukwea kileleni lakini kwa kiasi kikubwa Rooney amekuwa
akiendelea kufanya vizuri na kuonyesha kiwango kikubwa.
Lakini hata
Koke wa Atletico anayeongoza Ulaya, timu yake siyo inayofanya vizuri kuliko
Barcelona, Madrid na Atletico Madrid lakini kwa uwezo wake, ameendelea kufanya
vizuri zaidi.
WAKALI
ULAYA
TIMU PASI
|
|
WAKALI
ENGLAND
|
|
TIMU
|
PASI
|
|
|
6
|
|||
|
6
|
|||
|
5
|
|||
|
5
|
|||
|
5
|








0 COMMENTS:
Post a Comment