December 28, 2013



 
MWOMBEKI (KUSHOTO) AKIITUMIKIA SIMBA
Kocha Msaidizi wa Simba, Selemani Matola amesema mshambuliaji Betram Mwombeki hajawahi kufukuzwa.
 
Matola amesema mara nyingi imeelezwa Mwombeki ametemwa, lakini usahihi ni kutopata na nafasi ya kucheza kutokana na mfumo mpya wa kocha.

“Unajua kocha ameanzisha utaratibu mpya wa wachezaji. Nitakupa kwa mfano, ameteua wachezaji 25, hiki ndiyo kikosi chake.
“Tunapokwenda kwenye mechi anaweza kusema anataka wachezaji 20 tu, zaidi ya hapo wanapumzika. Tukirudi mazoezi nao wanarudi.
“Baada ya kuanza maandalizi upya tena inategemea kila mmoja anamridhisha vipi kocha na anaweza akarudi na yule aliyekuwepo asipangwe au kuingia kwenye benchi.

“Hii si kufukuzwa badala yake ni kupanda na kushuka katika kikosi na kila mchezaji anapaswa kujituma ili kupata nafasi,” alisema Matola.
Hivi karibuni kulikuwa na taarifa huenda Mwombeki ametemwa katika kikosi cha Logarusic ambaye amekuwa kocha asiyetaka mzaha.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic