December 13, 2013





Kocha Msaidizi wa Yanga, Felix Minziro amemwambia aliyekuwa Kocha Msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ apunguze kuzungumza, badala yake afanye kazi.


Julio hivi karibuni alitimuliwa na Simba pamoja na aliyekuwa Kocha Mkuu, Abdallah Kibadeni ambaye sasa ametua Ashanti United.

Minziro amesema Julio ana uwezo mkubwa wa kufundisha, kikubwa kinachomponza ni kelele anazozipiga kitu ambacho siyo sahihi.

“Nampa ushauri wa bure mdogo wangu Julio, ili adumu kwenye timu zetu za Bongo muda mrefu, basi aache kelele, badala yake afanye kazi pekee, ninaamini atafanikiwa zaidi ya hapo alipo.

“Julio ana uwezo mkubwa wa kufundisha soka, anaingia kwenye orodha ya makocha bora nchini kutokana na uwezo wake mkubwa, kama akiufanyia kazi ushauri wangu, atafika mbali,” alisema Minziro.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic