Yanga imemjumuisha Kocha Zdravko
Logarusic wa Simba katika idadi ya makocha inaowataka.
Habari za uhakika zimeeleza Yanga
imemjadili kocha huyo na huenda ikafanya naye mazungumzo ili asitishe mkataba
wake wa miezi sita Simba na kutua Jangwani.
Ingawa viongozi wa Yanga wamekuwa
wagumu kulizungumzia suala la kocha mpya baada ya kumtema Ernie Brandts, lakini
Logarusic ni kati yao.
“Kweli kabisa, Yanga wamevutiwa na kazi
ya Logarusic na wanaamini ana uwezo wa kuwathibiti mastaa wa Yanga.
“Hivyo wamempa mtu kazi ya kuwasaidia
kuzungumza naye na ikiwezekana mara moja ajiunge na timu hiyo.
“Unaweza ukasikia wakati wowote amechukuliwa
na kuanza kuifundisha timu hiyo,” kilieleza chanzo cha uhakika.
Juhudi za kumsaka Logarusic akiwa
nchini kwao Croatia kwa ajili ya mazungumzo zilifanikiwa na alisema hivi:
“Naiheshimu Yanga, lakini naheshimu
zaidi mkataba wangu wa miezi sita na Simba, sasa imebaki miezi mitano. Sipendi
kuzungumzia timu nyingine kwa kuwa mimi ni mtu ninayefuata weledi,” alisema
Logarusic bila kukataa au kukubali kama amefanya mazungumzo na Yanga.
Imeelezwa viongozi wa Yanga
wamefurahishwa na kazi yake siku Simba ilipoilamba Yanga kwa mabao 3-1 katika
mechi ya Nani Mtani Jembe, huku akionyesha hajali nani ni staa kwenye timu na
aliyeharibu, mara moja alisukumizwa kwenye benchi.
kwani hao yanga kwann wanapenda sana kuwachimba simba kwann wasitafute kocha wao wenyewe kwann wangoje simba wawaletee ndo wachukue au wanamatatizo ya akili?
ReplyDelete