December 11, 2013

NIKIWA NA MZEE SMALL MAENEO YA TABATA, KARIBU KABISA NA NYUMBANI KWAKE. HII ILIKUWA  LEO MCHANA.

Said Ngamba maarufu kama Mzee Small amesema kweli anaumwa lakini amekuwa akiendelea kujiuguza.


Mzee Small alizushiwa kifo kupitia mitandao ya kijamii ya Twitter na Facebook jana usiku, amesema alizipokea taarifa hizo kwa mshangao.

“Kweli inashangaza, vipi watu waamue tu kukuzushia eti umekufa, wameuliza wapi na nani kawaeleza, kitu cha ajabu sana.

“Lakini nipo na Mungu ndiye anapanga, siku ya mwisho atatoa jibu kuhusiana nami kwamba mwisho umefika au la,” alisema.
SALEHJEMBE ilimtembelea Mzee Small hadi nyumbani kwake Tabata jijini Dar es Salaam na kusema amekuwa akiendelea na mazoezi.
NIKIWA NA MZEE SMALL NA MKEWE MAMA SAID TUKIELEKEA NYUMBANI KWAO AMBAKO NILIKUNYWA SOKA KAMA MGENI...HEHE

“Nafanya mazoezi kwa ajili ya kujiimarisha zaidi kiafya, ni kazi ngumu lakini najitahidi kwa kuwa upande mmoja wa mwili wangu hauna nguvu, naweza kusema umepooza,ndiyo maana wakati mwingine nalazimika kutumia fimbo ili kutembea vizuri,” alisema.

Taarifa za Mzee Small kwamba amefariki dunia ziliwachanganya wengi hadi SALEHJEMBE ilipoandika na kueleza haikuwa kweli.
Mkewe Mzee Small naye pia alisema walishitushwa na taarifa hizo ambazo hawakuwa wamejua zimetokea wapi.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic