December 20, 2013



 

Klabu ya Yanga imeingia mkataba na Kampuni ya MGB Agency ya Zamalek, Cairo ya kuuza mechi yao ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya El Ahly ya nchini Misri ikiwa watasonga mbele katika hatua ya awali ya michuano hiyo.


Mechi hiyo ya mzunguko wa pili wa michuano hiyo, kama Yanga itafanikiwa kuwaondoa wapinzani wao Komorozine ya Comoro, itachezwa Januari 16, mwakani kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu wa Yanga, Beno Njovu, amesema mechi hiyo wameiuza kwa dola 55,000 (Sh milioni 88).

Njovu alisema mkataba huo walioingia nao ni kwa mechi moja pekee itakayochezwa Dar es Salaam.

“Tumeiuza mechi yetu ya mzunguko wa pili mara tutakapovuka na kukutana na wapinzani wetu El Ahly, tumeiuza kwenye Kampuni ya MGB ya nchini huko. Hivi sasa tupo kwenye mazungumzo na televisheni tutakayoipa tenda ya kurekodi mechi hiyo na kuirusha moja kwa moja Misri,” alisema Njovu.

Kwa upande wa mwakilishi wa kampuni hiyo, Francis Gaitho, alisema kuwa tofauti na Misri nchi nyingine zitakazotazama mechi hiyo ni zilizopo Ukanda wa Afrika Magharibi na Afrika ya Kati.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic