January 27, 2014


Kocha wa Ashanti, Abdallah Kibadeni, ameponda kiwango hafifu kilichoonyeshwa na Yanga walipocheza nao kwenye mechi ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara juzi Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Yanga na Ashanti ziliumana juzi ambapo mabingwa hao watetezi waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 huku wakionyesha kiwango cha chini tofauti na mashabiki walivyotegemea.

 Kibadeni amesema mechi yao na Yanga ilikuwa nyepesi sana.
Alisema Yanga ya mzunguko wa kwanza ilikuwa nzuri tofauti na hii ya sasa, ndiyo maana hata ushindi wao wameupata kwa shida.

Aliongeza kuwa, kilichowafanya vijana wake wapoteze mchezo huo ni kukosa umakini, pia kuna baadhi ya wachezaji wake walikuwa wazito sana uwanjani na alipofanya mabadiliko ndipo wakafanikiwa kuwadhibiti wapinzani wao na kuweza kupata bao hilo moja.
“Hawa Yanga mbona wepesi sana, wachezaji wao wengi wanajiamini jambo ambalo katika mpira halitakiwi lakini nawapongeza kwa kuwa wamepata pointi tatu na zitawasaidia, licha ya hivyo wasibweteke,” alisema Kibadeni. 







1 COMMENTS:

  1. hizo mbwembwe tumezizoea kwa makocha wa kitanzania. Badala ya kuongea kiufundi wanaleta siasa na ndio maana hatusongi mbele

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic